Potatoe - Dar East Project

Post Top Ad

Potatoe

Potatoe

Share This
 UTANGULIZI
Viazi mviringo ni zao muhimu la chakula na biashara katika nchi nyingi zinazoendelea. viazi husitawi vizuri sehemu zenye miinuko kati ya mita 1300 hadi 2700 juu ya usawa wa bahari. hukomaa katika kipindi cha miezi mitatu hadi mitano.
viazi mviringo vina virutubisho  vingi mfano vitamin, protin,madini na maji


           SIFA ZA MBEGU BORA ZA VIAZI

    Zenye kutoa mazao mengi zaidi kutoka kwenye shina moja
    ziwe zimechipua vizuri na ziwe na machipukizi mengi zaidi ya manne
    zisiwe na wadudu pamoja na magonjwa
    zitoke katika aina ambayo haishambuliwi na magonjwa kama vile ukungu na mnyauko
    zenye ukubwa wa wastani unaolingana na ukubwa wa yai la kuku

 
 
 mfano wa viazi mviringo

AINA BORA YA VIAZI MVIRINGO
Kuna aina nyingi sana ya viazi mviringo lakini hapa nitataja aina ambazo nazifahamu na ni bora
kutoka taasisi ya utafiti wa kilimo uyole

    baraka
    sasamua
    tana
    subira(EAI 2329)
    Bulongwa
    kikondo(CIP 720050)


      MUDA WA KUPANDA
Viazi mviringo mara nyingi katika maeneo mengi vinapandwa agost hadi september na november hadi december
  Natumia sentimita 60 hadi 75 kutoka mstari hadi mstari na nafasi kati ya kiazi na kiazi ni sentimita 30.

   MBOLEA
Ili kupata mazao mengi kutoka shambani mkulima anashauriwa kutumia mbolea aina ya samadi, mboji, maan mabichi  na za viwandani

kwa mbolea za viwandani tumia kilo 300 au mifuko 6 za mbolea ya TSP kwa hekta moja, ns kilo 300 mifuko 6 za mbolea ya CAN au kilo 400 mifuko 8 ya SA au kilo 175 mifuko 3.5 za UREA.

  PALIZI
Palilia viazi wiki mbili au tatu baada ya kuchomoza. inulia udongo kufanya tuta zuri ili pawepo na unyevu wa kutosha na kufunika viazi kutokana na mwanga wa jua

MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU
Ili kuzuia ugonjwa wa ukungu tumia Ridomil.
changanya gram 100 za dawa  katika lita 20 za maji na nyunyuzia mara baada kila wiki mbili au tatu kutegemea na hali ya hewa.
nyunyuzia dawa ya karate kiasi cha mililita 20 mpaka 40 za dawa katika lita 20 za maji ili kuzuia wadudu kama inzi weupe na wengine. Tumia mbinu bora za kilimo kama usafi wa shamba au kilimo mzunguko kama mbinu ya kuzuia magonjwa na wadudu.

KUVUNA NA MAVUNO

Viazi huwa tayari kuvunwa baada ya miezi 3 hadi 5 kutoka kupanda. mda wa kuvuna unategemea na mda wa kupanda na dhumuni la zao
usiache viazi shamban bila kufunika  kwa nyasi au udongo  kwa mda mrefu

KUHIFADHI
Viazi vya chakula viiafadhiwe kwenye ghara hewa ya kutosha pasiwe na unyevunyevu na joto kali

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here